• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

WAFANYABIASHARA WA MAZAO NA WENYE MAGHALA KUSAJILIWA KIDIGITALI

Posted on: July 6th, 2023

WAFANYABIASHARA WA MAZAO NA WENYE MAGHALA KUSAJILIWA KIDIGITALI

Mkuu wa wilaya ya Mpanda mhe Jamila Yusuph amewataka Wafanyabiashara wa mazoa waliopo wilaya ya mpanda kutoa ushirikaiano kwa maafisa wa Serikali watakaopita kwenye biashara zao ili kutekeleza zoezi la usajili wa biashara ikiwa ni  utekelezaji wa zoezi la urasimishaji wa biashara zao ili kuendana na na matakwa ya  Wizara ya Kilimo ambayo yanamtaka kila mfanyabishara wa mazoa kurasimiasha biasahara yake.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya mapema leo Julai 6, 2023 katika kikao chake na wafanyabiashara kilichofanyika katika ukumbi wa Manispa ya Mpanda kikiwa na  lengo la kuwaeleza zoezi la  Urasimishaji wa Biashara ya mazao ya Kilimo kwa kuboresha utaratibu wa Uuzaji na Ununuzi wa Mazao ya Kilimo nchini ambapo utaratibu huo unasimamiwa na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Aidha Mhe Jamila elmeeleza kuwa  Lengo serikali la kuboresha Utaratibu huu ni pamoja na Kuwalinda wakulima na wafanyabiashara dhidi ya usumbufu na utapeli unaotokea katika biashara ya mazao ya kilimo, Kurasimisha Sekta ya Kilimo Mazao ili kuwezesha ufanyaji biashara kwa mujibu wa sheria na taratibu, Kuwalinda wafanyabiashara wa ndani dhidi ya wafanyabiashara kutoka nje ya Tanzania wanaonunua mazao moja kwa moja shambani, Kuwasaidia wakulima wa Tanzania kunufaika kutokana na jitihada za Serikali za kutoa ruzuku na uwekezaji unaoendelea ili kupunguza gharama za kilimo na kuongeza uzalishaji Pamoja na Kuwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi za biashara ya mazao ya kilimo ikiwa ni pamoja na kujua hali halisi ya usalama wa chakula nchini.   

  • Akiwasilisha taarifa ya namna zoezi litakavyoendeshwa Gwalusajo Kapande ambaye ni  Mkuu wa Idara ya Kilimo,  kwa niaba ya Mkurugenzi emeeleza kuwa ili kuhakikisha biashara ya Mazao ya Kilimo inarasimishwa nchi nzima, Wizara ya Kilimo imetengeneza Mfumo Maalum wa Kielektroniki (Kidigali) utakaotumika nchi nzima. Hivyo katika kuutekeleza Mfumo huu kwa Ufanisi ni lazima mambo matano ya msingi yazingatiwe, ambayo ni Usajili wa Maghala, Usajili wa Wafanyabishara ya Mazao ya Kilimo, Usajili wa Masoko ya Mazao ya Kilimo, Usajili ya Vituo vya Ununuzi Pamoja na Usajili wa Vituo vya Ukaguzi Mazao ambapo njia kuu mbili za usajili zitatumika ambazo ni usajili kupitia tovuti  ya https//asds.kilimo.go.tz  au kwa kutumia kilimo APP

Mhe Jamila ameeleza kuwa Ili serikali iweze kutimiza malengo iliyojiwekea na ili wafanyabiashara waweze kuuza au kununua mazao katika Halmashauri ya Manispaa ya  Mpanda wanatakiwa fanya mambo yafuatayo:

 

Wafanyabiashara wote wa Mazao ya Kilimo ni lazima “Wanunulie na Kuuzia” Mazao yao kwenye Vituo maalum Vilivyoainishwa na si vinginevyo.

Wafanyabiashara wote wahakikishe wanatumia Mizani katika Kununua Mazao ya Kilimo. Aidha Mizani hizo ni lazima ziwe zimethibitishwa ubora na Wakala wa Vipimo.  

Wafanyabiashara wote wa mazao ya kilimo ni Lazima wasajiliwe na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ili kuwatambua na pia kuwa na Takwimu sahihi za Mazao yote yaliyouzwa na kununuliwa kupitia wao. Aidha hakuna gharama yoyote ya Kusajili “NI BURE”.

Wanunuzi wa mazao kutoka nje ya nchi Ni lazima wanunue Mazao yao kupitia kwa wafanyabiashara wa mazao ya kilimo waliosajiliwa Manispaa na siyo kununua mashambani. Aidha Mfanyabiashara yeyote wa Kigeni akikamatwa ananunua Mazao Kijijini kwa Wakulima, Hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.  

Ghala zote zinazohifadhi mazao ya kilimo nchini (binafsi, ushirika, Serikali) zitasajiliwa kupitia mfumo wa Kielektroniki na kupatiwa namba maalumu ya utambulisho bila gharama yoyote. Aidha, kila mfanyabiashara wa mazao ya kilimo hapa nchini atalazimika kutoa taarifa ya kiasi cha mazao yaliyonunuliwa, yaliyohifadhiwa na kuuzwa kupitia mfumo huo

Mfanyabiashara anayesafirisha mazao ya kilimo ndani ya nchi atapaswa kupata kibali cha kusafirisha mazao (movement order) kutoka ofisi za wakuu wa Wilaya husika. Kibali hicho kitawawezesha wafanyabiashara kusafirisha mazao kutoka Wilaya moja kwenda nyingine na kutoka Mkoa mmoja kwenda mwingine; Kibali kitatolewa Bure Kabisa.  

Wafanyabiashara wote wanakumbushwa kuwa ni marufuku kutumia madalali wakati wa kuomba vibali vya kusafirisha mazao ya kilimo nje ya nchi, bali waombe moja kwa moja kupitia mfumo wa ATMIS au kufika kwenye Ofisi za Wizara ya Kilimo kwa msaada zaidi; na

Wafanyabiashara wa mazao ya kilimo wenye Mikataba maalum ya kununua mazao kwa wakulima Ni lazima wawasilishe nakala za mikataba hiyo Ofisi za Manispaa ya Mpanda kwa ajili ya kufanyiwa uhakiki.

Akizungumza mbela ya Mkuu wa Wilaya Ally Seif ambaye ni mfanyabiasha wa mazao na mmiliki wa ghala kwa niaba ya wafanyabiasha ameishukuru serikali kwa kuanzisha utaratibu huu wenye lengo la kumlinda mkulima na  mfanyabiashara wa ndani. Amewasihi wafanyabiashara wenzake kulipokea zoezi hilo kwa mtazamo Chanya na kuwataka kwenda kwenye utekelezaji.

Aidha wafanyabiashara wamemuomba  Mkuu wa wilaya baada ya mwezi mmoja wa utekelezaji aitishe kikao cha tathimini ili kuona na kutatua changamoto zitakazokuwa zimejitokeza wakati wa utekelezaji jambo ambalo lilikubaliwa na mkuu wa wilaya ambapo kikao cha tathimini kitafanyika Agosti 15, 2023.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.