• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

Posted on: June 19th, 2025

SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Mpanda Mhe. Haidary Sumry amesema serikali kwa kipindi cha miaka Mitano kuanzia Mwaka 2020/2025 imeleta fedha kiasi zaidi Bilioni 29 kwaajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akitoa taarifa kwa wandishi wa Habari Mkoa wa Katavi Sumry amesema kuwa kwa kipindi cha Miaka mitano katika Manispaa ya Mpanda kumekuwa na mwendelezo wa kuleta fedha za miradi ya maendeleo kwa kiwango kikubwa hali ambayo imepelekea kuimarika kwa huduma za wananchi kupitia fedha za maendeleo.

Amesema kuwa kiasi hicho cha fedha kimekuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi kupitia sekta ya Elimu,Afya,miundombinu na Maji kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wanachi.

Katika sekta ya Elimu Msingi kwa kipindi cha Miaka Mitano iliyopita kupitia fedha mbalimbali za serikali Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kujenga Shule za Msingi mpya tano zenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.5 kwenye shule hizo tano Halmashauri imefanikiwa kujenga Shule ya msingi ya mchepuo wa kiingereza.

Kuhusu ujenzi wa Madarasa kwenye Elimu ya Msingi Sumry ameeleza kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kujenga vyumba vya madarasa 128 vye thamani ya shilingi bilioni 3.6

Kwenye eneo la miundombinu ya Madarasa kwa kipindi cha Miaka mitano Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda katika kukabiliana na upungufu wa Madawati kwenye eneo la Elimu Msingi Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kutengeneza madawati 3310 pamoja na kujenga matundu ya vyoo 154 yenye thamani ya Shilingi Milioni 180.

Katika upande wa Elimu Sekondari Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kujenga Sekondari Mpya Katika Kata ya Mwamkulu,na Nsemlwa pamoja na kuongeza Sekondari mpya za sekondari kwenye baadhi ya kata ikiwemo Kata ya Kazima,na Kata ya Shanwe pamoja na Kata ya Nsemlwa.

‘’Kwahiyo kama Manispaa kwa kipindi cha miaka mitano tumefanikiwa kujenga Sekondari mpya Nane zenye thamani ya Shilingi Bilioni 7.1’’ anasema Sumry .

Katika eneo la ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye Elimu Sekondari amesema kuwa wamefanikiwa kujenga vyumba vya Madarasa 55 yenye thamani ya Shilingi Bilioni1.2 pamoja na kutengeneza viti na meza 2160 zenye thamani ya shilingi Milioni 151.

Katika hatua nyingine Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda katika eneo hilo la Ellimu ya Sekondari imefanikiwa kujenga matundu ya vyoo 38 kwa gharama ya shilingi Milioni 75 pamoja na kufanikiwa kujenga Mabweni Nane kwa Gharama ya shilingi Milioni 827.

Katika eneo la Sekta ya Afya Mstahiki Meya Sumry amesema kwa kipindi cha miaka mitano wameweza kufanya ukarabati wa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda kwa Gharama ya Milioni 900 huku wakifanikiwa kujenga vituo vya afya vitatu vyenye Thamani ya Shilingi Bilioni 1.5 huku kituo kimoja kipombioni kuanza kujengwa Kata ya Misunkumilo.

Kuhusu ujenzi wa Zahanati amesema Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kujenga Zahanati tano zenye thamani ya shilingi milioni 560.

Katika Sekta ya Kilimo Sumry ameipongeza serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuimarisha sekta ya Hususani eneo la Kilimo cha umwagiliaji ambapo kwa kipindi cha miaka mitano Manispaa ya Mpanda imefanikiwa kupata mradi wa kilimo cha umwagiliaji kata ya mwamkulu wenye thamani ya shilingi Bilioni 31 ambao unaendelea kujengwa.

Amesema kuwa kwa namna ya pekee anamshuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi hicho cha fedha cha Zaidi ya Bilioni 29 kuzileta Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi kwaajili ya kusaidia kutatua kero za wananchi kupitia ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

    June 19, 2025
  • SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

    June 19, 2025
  • MADIWANI WAAGA RASMI

    June 19, 2025
  • MADIWANI WAAGA RASMI

    June 19, 2025
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.