• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

BARAZA LA MADIWANI LAADHIMIA KUTOIPOKEA ILIYOKUWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA KATAVI.

Posted on: February 1st, 2023

BARAZA LA MADIWANI LAADHIMIA KUTOIPOKEA ILIYOKUWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA KATAVI.

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda limeadhimia kutoipokea Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambayo awali ilikuwa inatumika kama hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi. 

Kauli hiyo imetolewa Jana Tarehe 31,01,2023 katika kikao cha Baraza la madiwani baada ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Dkt. Paul Swakala kueleza kuwa suala la uondoshaji wa baadhi ya vifaa tiba na vifaa vingine katika hospital hiyo linakwenda kinyume na utaratibu.

Dr. Swakala ameliomba Baraza la Madiwani kuingilia kati suala hilo kwani endapo tutakakabidhiwa hospitali hiyo ambayo itakuwa haina vitendaa kazi tutashindwa kuwahudumia wananchi kutokana na baadhi ya vifaa muhimu kuondolewa tena bila utaratibu wa makabidhiano.

Akiongea kwa masikitiko makubwa Diwani wa Kata ya Majengo Mhe. William Mbogo ameeleza kuwa Manispaa ya Mpanda iliikabidhi hospitali hiyo kwa nyaraka maalumu (M.O.U), na kwamba kitendo cha kuondosha vifaa tiba na vifaa vingine bila makabidhiano wala bila nyaraka ni kinyume na utaratibu.

"Mimi ninavyofahamu hospitali ya Rufaa hupokea wagonjwa kutoka Hispatali za Wilaya, sasa unapobeba vifaa vyoye muhimu tafsiri ni kwamba umeiondolea uwezo hospital ya wilaya na hivyo utasababisha msongamano kwenye hospital ya Rufaa. Tuombe mamlaka za juu kuingikia kati swala hili ambalo linafanyika kinyume na utaratibu"- Alisema Mbogo diwani wa kata ya Majengo.

Naye Askofu Labani Ndimubenya ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya afya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda alieleza wazi kuwa zipo taarifa na lakini pia amekuwa akishuhudia baadhi ya vitu kama vitanda, makabati, viti, komputa pamoja na vifaa vingine vikihamishwa kutoka hospitali hiyo kupelekwa hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Katavi.

“Serikali yetu ni moja, inamhudumia mwananchi huyohuyo, sasa sioni sababu ya serikali kwa serikali kuvutana, kwekweli kitendo ambacho kinafanyika pale hospitali sio cha kiungwana, vitu vinahamishwa kienyeji, ukibeba vitanda, meza, komputa hawa watakaobaki watatoaje huduma?” Alisema Askofu Labani Ndimubenya mjumbe wa bodi ya afya

Kufuatia hali hiyo, Baraza la Madiwani limeadhimia kumwandikia Barua Katibu Tawala Mkoa wa Katavi ili aweze kuingilia kati mgogoro huo wa makabidhiano na uweze kufika muafaka.

Aidha baraza limeeleza wazi kuwa halitakuwa tayari kuipokea hospital hiyo kama makabidhiano pamoja na mgawanyo wa mali hautofanyika kwa kufuata utaratibu.

Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda awali ilitumika kama hospitali Teule ya Rufaa Mkoa kabla Hospitali ya mkoa kujengwa hivyo baada ya Hospitali hiyo kuanza kazi utaratibu ukawa ni Hospitali hizo mbili kugawana baadhi ya vifaa.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.