• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

DC Mpanda uzindua zoezi la ugawaji wa vitabu vya miongozo ya Elimu.

Posted on: September 14th, 2022

DC Mpanda  uzindua zoezi la ugawaji wa vitabu vya miongozo ya Elimu.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe Jamila Yusuph amefanya uzinduzi wa ugawaji wa vitabu vya miongozo ya Elimu. Uzinduzi huo umefanyika mapema leo katika kiako cha wadau wa elimu wa Manispaa ya Mpanda kilichofanyika kaitika ukumbi wa mikutano wa Manispaa.(Mpanda Municipali Social Hall)

Akiongea katika kikao hicho Mhe. Jamila alieleza kuwa, Ili miongozo hii ilete matunda tarajiwa inapaswa kueleweka vizuri na wadau wa elimu wa ngazi zote ikiwemo ngazi ya shule na jamii, aidha Miongozo hii imeanisha masuala mbalimbali yakielimu ikiwamo changamoto na utatuzi wake ili kuboresha utoaji wa elimu ya msingi na sekondari.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ndugu Deodatus C Kangu ikitoa taarifa kwa mgeni rasmi mbele ya wadau wa elimu ameeleza kuwa, Miongozo hii imelenga kuthibiti utoro wa wanafunzi ambao ni kikwazo kikubwa katika ufundishaji na ujifunzaji ambapo  Maafisa Watendaji wa Kata/Mitaa wanapaswa kushughulia utoro kwa kutoa Elimu kwa jamii kupitia vikao na nyumba za ibada kuhusu sheria ya elimu na. 25 ya 1978 inayo eleza kuwa anaye sababisha mwanafunzi kutohudhuria shule atafungwa jela miezi 6 au kutoa faini kati ya shilingi 30,000 hadi 50,000.

 

Mwalimu Mkuu/Mkuu wa shule ahakikishe kuwa a)Wanafunzi wanaitwa majina mara 2 kwa siku. b)Kumwita mzazi shuleni iwapo mtoto wake hata hudhuria shuleni siku 2 mfululizo ili atoe maelezo.

Afisa Elimu Kata kila wiki atapokea majina ya wanafunzi ambao hawakuhudhuria shuleni siku 5 mfululizo na kuyapeleka kwa WEO kwa hatua tajwa hapo juu. WEO atatakiwa kuchukua hatua na kutoa taarifa ya utekelezaji kwa DC, MD na Afisa Tarafa

Aidha muongozo utasaidia kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu ya msingi. Ili kuimarisha ufundishaji inaelekezwa Kila Kata iwe na Kamati ya Elimu ya Kata (KAEKA). Mhe. Diwani atakuwa M/kiti, AEK katibu, wajumbe ni WEO,VEO,Wenyeviti wa Mitaa, kamati za shule na Walimu wakuu/Wakuu wa shule.

Kamati itafanya kikao cha KAEKA Kila baada ya miezi 3 kinacho tanguliwa na ziara katika shule zote katani Kubainisha changamoto za kielimu na kuzipatia ufumbuzi. Miongoni mwa changamoto hizo zaweza kuwa ni upungufu wa miundombinu, utoro, mdondoko, wanafunzi kutopata chakula cha mchana shuleni, unyanyasaji wa kijinsia.

Muongozo huu utasaidia kuondoa upungufu wa miundombinu ambapo Mkakati unaelekeza kuondoa upungufu wa miundombinu na msongamano darasani kwa kuwatumia wadau na jamii,  Inaelekezwa kuwa

1.Kila mwaka jamii inayoizunguka shule kupewa malengo ya ujenzi wa maboma ya vyumba viwili vya madarasa/Utengenezaji thamani

2.Halmashauri kutenga katika bajeti ya maendeleo 10% ya mapato ya ndani kwaajili ya kumalizia miundombinu ya shule kila mwaka

3. UJenzi kuwa moja ya kipimo cha utendaji wa MD, WEO na VEO

Muongozo huu utasaidia kuondoa changamoto ya ukosefu wa chakula ambapo usala la chakula shuleni itakuwa lazima. katika kutekelea jambo hili WEO,VEO na Kamati za shule zitaunda kamati za kusimamia chakula na ziandae mpango shirikishi kuwezesha uchangiaji chakula.

 

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda alihitisha kwa kusema kuwa ili miongozo hii ilete tija tarajiwa inapaswa kuwafikia wadau wote kwa utekelezaji hivyo alielekeza mambo yafuatayo:-

1. Maafisa Elimu Kata na Walimu Wakuu kuhakikisha Kamati/Bodi za shule na kwa kipekee walimu wote wanapitishwa katika vipengele vya miongozo ikiwemo utatuzi wa utoro wa walimu.

2. Maafisa Watendaji wa Kata wahakikishe wazazi/jamii inapitishwa katika maeneo ya mwongozo ikiwemo kukomesha utoro na kuchangia maendeleo ya shule.

3. Ofisi zote za kata ziandae vikao vya kuelezea miongozo hii kwenye kata zao.

Baadhi ya wadau wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, wameishukuru serikali kwa kuandaa na kuzindua miongozo itakayosaidia kuinua sekata ya elimu, aidha wameeleza kuwa kwa kuanzisha sula la la chakula shuleni kuwa lazima litasidia watoto wetu kuboresha afya zao pamoja na  kupata nafasi ya kujifunza kwa utulivu bil kuwa za njaa.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.