• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

Kampeni ya chanjo Katavi Kufanyika kikamilifu

Posted on: September 11th, 2019

Wakazi wa mkoa wa Katavi wanatakiwa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kwa kuwapeleka watoto wao wenye umri chini ya miaka 5 kwenye vituo vya Afya, zahanati na maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya kutoa chanjo ya kukinga magojwa ya Surua, Polio na Rubella.

Hayo yamebainishwa na mkuu wa Mkoa wa Katavi Comrade Juma Z. Homera katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mapema leo ofisini kwake. RC Homera elieleza kuwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na wadau imeandaa kampeni ya kitaifa ya kutoa chanjo za Surua, Rubella na Polio. Kampeni hii yenye kauli mbiu isemayo“Chanjo ni kinga; Kwa pamoja tuwakinge” itafanyika kwa utaratibu wa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano kupewa chanjo.

Aidha alifafanua kuwa lengo mahususi la kampeni hii ya kitaifa ni kuzuia na kupambana na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ambayo ni ugonjwa wa Surua, Rubela na Polio kwa kutoa chanjo kwa watoto wote wenye umri  chini ya miaka 5 pamoja  kuongeza kinga kwa watoto wote kwa kuwapatia chanjo hata kama wameshapata chanjo hizo katika utaratibu wa kawaida wa kutoa huduma za chanjo.Kampeni itafanyika kitaifa kwa siku tano (5) kuanzia Alhamisi tarehe 26 hadi Jumatatu tarehe 30 Septemba,2019 . Siku hizi zitatumika kutoa chanjo kwa watoto wote waliolengwa

RC Homera amewataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliolengwa wanapata chanjo kwa kuwa  Magonjwa ya Surua na Rubella  hukingwa kwa chanjo ya Surua-Rubella. “Ni muhimu kwa mzazi kuhakikisha mtoto anakamilisha chanjo zote ikiwemo chanjo ya marudio ya Surua-Rubella ili kuimarisha kinga” Alisema RC Homera. Mtoto anapougua Surua au Rubella apelekwe mapema kituo cha afya kwa matibabu na ushauri. Mtoto mwenye Surua au Rubella apewe vinywaji na chakula cha kutosha. Chanjo hizi ni salama zimathibitishwa na shirika la Afya Duniani na Wizara ya Afya.

“Chanjo hutolewa bila malipo katika vituo vyote vya serikali na watu bianafsi. Utamkinga mtoto wako na maisha yake ya baadae kwa kuhakikisha anakamilisha ratiba ya  chanjo .Mtoto asiyekamilisha ratiba ya chanjo ni hatari kwa maisha yake na jamii inayomzunguka kwani ni rahisi kuambukizwa  magonjwa na  kuambukiza wengine” Alisema RC Homera. Aidha amewatahadharisha wote watakao jaribu kupotosha au kuihujumu serikali kwa kukwamisha kampeni hii kuwa watachukuliwa hatua za kisheria

 

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.