KASI, UBORA, NA MATUMIZI YA FEDHA MIRADI YA BOOST YAMFURAHISHA RC RUKWA
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi Makongoro Nyerere amesema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa ya mradi wa ujenzi wa shule mpya ya msingi Nyerere unaojengwa kwa fedha za BOOST kwa thamani ya shilingi milioni 561 na laki moja.
RC Nyerere ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi ya shule zinazojengwa kwa fedha za BOOST ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo ambapo licha ya kuridhishwa na hatua ya ujenzi wa mradi wa shule mpya ya msingi Nyerere pia amesema tayari hatua iliyofikiwa thamani ya fedha inaonekana huku akitaka usimamizi zaidi ili mradi huo ukamilike kwa wakati.
Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mwalimu mkuu Shule ya msingi Nyerere, Zuhura Kapama amesema shule hiyo mpya itakuwa na Vyumba 16 vya madarasa (Vyumba 14 vya elimu msingi na viwili vya elimu ya awali), matundu 26 ya vyoo na jengo la utawala.
Mwalimu Kapama amesema kumamilika kwa shule hiyo kutapunguza changamoto ya msongamano wa wanafunzi wa shule ya msingi mama (Nyerere), kutoka wanafunzi 553 kwa darasa mpaka wanafunzi 128 kwa madarasa.
Amesema hadi sasa shule ya msingi Nyerere inawanafunzi 4424 wa shule ya chekechea hadi darasa la Saba.
Kwa upande wao Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli na mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi bilioni 1.9 ambazo zitakwenda kukamilisha vyumba vya madarasa 61 ndani ya Manispaa hiyo.
Mradi mwingine ambao RC ameutembelea ni ujenzi wa shule mpya ya msingi Mkapa ambayo inajengwa kwa thamani ya shilingi milioni 561 na hadi sasa miradi yote imefikia hatua ya upauaji na kueezeka bati.
Kwa mujibu wa miongozo shule hizo zinazojengwa kwa fedha za BOOST Nchini zinatakiwa kufikia Juni 30 mwaka huu ziwe zimekamilika na kukabidhiwa.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.