Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imeibuka mshaindi katika maonesho ya nanenane kwa mwaka 2018 kwa kushika nafasi ya pili ikitanguliwa na Halmashauri ya wilaya ya Iringa.
Maonesho hayo yanajumuisha Halmashauri zote za mikoa 7 zinazopatikana katika nyanda za juu kusikini.
Katika maonesho hayo Manispaa ya Mpanda imepata kikombe na zawadi nyingine ikiwa ni ishara ya kuwa mshindi wa pili kwa kutoa alimu ya kilimo, ufugaji, uvuvi na ujasiliamali.
Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw.Michael Francis Nzyungu wakati akikabidhiwa kikombe cha ushindi amesema kuwa Halmashauri yake imepata ushindi huo kutokana na ushirikiano mkubwa uliooneshwa miongoni mwa watumishi, madiwani na Sekretarieti ya Mkoa wa Katavi. Aidha amesema kuwa atahakikisha kuwa wanatekeleza jukumu lao la kuwapelekea wakulima wa vijijini teknolojia na pembejeo bora ili kuongeza tija katika shughuli za uzalishaji mali na kujenga uchumi wa Viwanda katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.
Maonesho ya nananene kwa mwaka 2018katika nyanda za juu kusini yalifugwa rasmi na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege ambapo alizitaka Mikoa kuendeleza shughuli za kilimo, ufugaji, uvuvi na ujasiliamali ili kuungana na Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli katika kutekeleza dhana ya viwanda. Aidha amezitaka taasisi zote zinazojihusisha na shughuli za kilimo, mifugo na uvuvi kuendelea kufanya tafiti, kuhamasisha kilimo chenye tija ikiendanda sambamba na matumizi sahihi ya pembejeo. Aidha maafisa ugani wameagizwa kuwatumikia wananchi kwa kutoa elimu ya kilimo, ufugaji na uvuvi ili wananchi wafanye kilimo chenye tija.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.