• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

Manispaa ya Mpanda yajipanga sekta ya elimu

Posted on: April 4th, 2018


Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imefanya mkutano wa wadau wa elimu tarehe 03/04/2018. Mkutano huu unajumuisha wadau mbalimbali wakiwemo wanafunzi wenyewe, walimu, wazazi pamoja na viongozi mbalimbali  wakiwemo Walimu Wakuu, Wakuu wa shule, Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Vituo vya Walimu (Klasta), TAHOSSA, Viongozi wa CWT, Katibu TSC  Wilaya, Wathibiti ubora wa shule, Maafisa Elimu Wilaya, madiwani,  pamoja na mheshimiwa Mkuu wa Wilaya. Aidha mkutano huu inahusisha viongozi wa dini, viongozi wa siasa, taasisi za kiraia na wafadhili mbalimbali wa elimu na wadau wengine.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga ambaye alikuwa  Mgeni rasmi katika kikao hiki aliipongeza Manispaa ya Mpanda  kwa kuitisha kikao hiki muhimu na kuwaomba viongozi na wadau wote wa elimu kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza ufaulu na hatimaye mkoa kurudi katika nafasi ya kwanza kitaifa.

Aidha mgeni rasmi aliwataka wazazi na jamii nzima  kuzingatia na kuutafasili  vizuri waraka wa elimu bure ili kila mmoja atimize wajibu wake. Alisisitiza kuchangia chakula mashuleni na mambo mengine yanayoamuliwa na bodi za shule ili wananfunzi wasome katika mazingiara mazuri ili waweze kufauru kwa alama za juu.

Mkutano huu huitishwa kwa malengo mahususi ya Kutathmini mafanikio ya mfumo shirikikishi wa ufuatiliaji elimu na tathmini katika elimu, Kutathmini vikao vya wadau wa Elimu vya mwaka 2017 ngazi ya kata na mitaa na mkoa kwa ujumla, Kutathimini matokeo ya Mitihani ya Kitaifa ya mwaka 2013,2014,2015, ,2016 na 2017 kwa Manispaa ya Mpanda na mkoa kwa ujumla, Kuwapatia taarifa mbalimbali wadau wa Elimu wa Manispaa ya Mpanda na mkoa kwa ujumla ili kuwaongezea kasi ya utendaji na hivyo kuendeleza mafanikio tuliyoyapata katika Halmashauri na  Mkoa wetu;

Aidha kikao hiki kina lengo la Kuongeza umoja, ushirikiano na upendo baina ya wadau wa elimu na viongozi wa Elimu katika Manispaa ya Mpanda na mkoa kwa ujumla kwa lengo la kuongeza ufanisi katika elimu.

Aidha kulifanyika majadiliano ya uwajibikaji yaliyohusisha wadau wote yalifanyika ili kuboresha sekta ya elimu katika Manispaa ya Mpanda na mkoa kwa ujumla, ambapo kwa kauli moja wadau wote waliazimia kila mmoja kwa nafasi yake kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano na ufanisi ili kuinua kiwango cha elimu.

Sambamba na hilo, Mkurugenzi wa wa Manispaa ya Mpanda alitoa taarifa ya mpango na mkakati waliojiwekea ili kuhakikisha wanaongeza ufaulu kwa mwaka 2018 katika madarasa ya awali hadi darasa la saba. Halimashauri imejipanda kuongeza kiwango cha ufaulu kwa darasa la saba kutoka asilimia  90.01 mwaka 2017 hadi asilimia 99 mwaka 2018 na darasa la nne kutoka asilimia 92.48 mwaka 2017 hadi asilimia 99 mwaka 2018.

Kikao hicho kilihitimishwa kwa zawadi zilizo andaliwa na ofisi ya mkurugenzi wa Manispaa ya mpanda kwenda kwa waalimu, wanafunzi, wazazi na wadau waliofanya vizuri zaidi kwa mwaka 2017 ambazo zilikabidhiwa na mgeni rasmi.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.