MANISPAA YA MPANDA YAKUSANYA 52% KWA KIPINDI CHA MIEZI SITA
Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda iliyopo mkoani Katavi imefikia 52% ya makusanyo katika kipindi cha miezi sita ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2022/23. Hayo yamebainishwa na Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Mhe. Haidary H Sumry Februari 2, 2023 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake na kusema kuwa hali hiyo imechangiwa na usimamizi bora wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo na watendaji wengine.
Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ilikadiria kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 2.8 kwa mwaka wa fedha 2022/23 ambapo mpaka sasa imekusanya shilingi bilioni 1.6
Aidha Sumry amesema kuwa kulingana na hali hiyo, halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imekadiria makusanyo ya shilingi bilioni 3.3 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24 na ana imani malengo yanaweza kufikiwa.
"Kama mnavyoona ni ongezeko kubwa lakini lisiwashitue kwa sababu kwa kupitia mapato yetu ya nusu mwaka yametuonesha kuwa kuna direction (mwelekeo) kwamba kama kwa nusu mwaka tumekusanya billion 1.68 tafsiri yake kwa kipindi cha pili cha miezi 6 iliyobaki hatuna mashaka kwamba tunaweza tukafikia malengo ya kukusanya karibia bilioni 3.2 au 3"
Katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Sumry amesema halmashauri imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali kwa umakini mkubwa akiitolea mfano miradi wa Sequip ambapo Halmashauri ilipewa milioni 940 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya 2 Moja ikijengwa kata ya Ilembo na nyingine ikijengwa kata ya Kakese ya shule zote mbili zimekamilika na zimepokea wanafunzi mwaka huu 2023.
Miradi mingine ni ujenzi wa Zahanati na vituo vya afya pamoja na kuchonga barabara mpya katika maeneo ambayo Halmashauri hiyo imepima viwanja.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.