Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Generali (Mst) Raphael Muhuga amefanya ziara katika ofisi ya ardhi ya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.
Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa akiwa ameambatana na kamati ya malalamiko ya mkoa aliwaeleza watumishi wa idara ya ardhi kuwa ameamua kufanya ziara hiyo ili kujionea halihalisi ya utendaji kazi wa idara hiyo pamoja na namna walivyojipanga ili kupunguza migogoro itokanayo na ardhi.
Aliwaeleza kuwa katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika 14/04/2018 katika viwanja vya azimio zaidi ya asilimia 80 ya malalamiko yaliyowasilishwa yanatokana na airdhi, hivyo amewataka watumishi hao kila moja kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni na taratibu za utumishi wa umma huku wakilenga kupunguza au kumaliza kabisa migogoro ya ardhi.
Aliendelea kueleza kuwa maeneo mengi katika katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda yana viwanja vilivyopimwa muda mrefu ambavyo haivijaendelezwa kwa mujibu wa sheria, hivyo alimtaka Mkurugenzi kufanya utambuzi wa maeneo hayo ili taratibu wa kuvifuta viwanja hivyo zianze mapema.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.