• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

RC KATAVI ARIDHISHWA NA UJENZI WA MADARASA MPANDA

Posted on: November 9th, 2022

RC KATAVI ARIDHISHWA NA UJENZI WA MADARASA MPANDA

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko ameridhishwa na hatua za ujenzi wa vyumba 51 vya madarasa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda. Mhe Mrindoko amefanya ziara ya ukaguzi wa vyumba 51 vya madarasa vinavyogharimu bilioni moja (1) na milionini 20 kwa ajili ya maandalizi ya kuwapokea kidato cha kwanza kwa mwaka 2023.

Mkuu wa mkoa amewataka  watumishi wa Umma  na wote wenye dhamana ya kusimamia miradi hiyo kuwa waadilifu, na kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati uliopangwa na kwa ubora na viwango vinavyotakiwa.

Rai hiyo imetolewa 10 Novemba 2022 wakati akikagua Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa ya Rais Samia katika Manispaa ya Mpanda ikiwa ni utekelezaji wa ratiba ya kamati ya ulinzi na Usalama Mkoani humo kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Kwa Sasa hivi tunafuatilia ujenzi huu wa madarasa ya Rais Samia ili kuhakikisha kuwa Ujenzi wa Madarasa yanakamilika ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora unaotakiwa.Maelekezo ya Mhe.Rais ni kukamilisha madarasa haya Tarehe 15 Desemba 2022 lakini sisi Mkoa wa Katavi tunasema tutakamilisha Ujenzi huu Tarehe 07 Desemba 2022 ili ile wiki moja iwe ni ya Waziri wa TAMISEMI kufanya ufuatiliaji na kumkabidhi Mhe.Rais.”Alisema Mkuu wa Mkoa Mrindoko.

Bi.Mrindoko ameipongeza Manispaa ya Mpanda kwa kusimamia vizuri Ujenzi wa madarasa ya Mhe.Rais Samia ambapo amewataka kuongeza jitihada zaidi ili kuhakikisha kuwa Ujenzi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa.

“Nyie Manispaa ya Mpanda mnaongoza kwa kuwa na vyumba vingi vya madarasa na mna vyumba 51 kati ya 119 na katika maeneo niliyopitia nimeridhishwa na hatua nzuri ya ujenzi hivyo msibweteke na sifa na badala yake mjipange kuhakikisha kuwa mnakamilisha Ujenzi ndani ya muda uliopangwa”alisema Bi.Mrindoko.

Aidha Bi Mrindoko ametoa rai kwa Wananchi kuendelea kuchangia nguvu kazi katika Ujenzi wa Madarasa 119 ili Shilingi Milioni Ishirini iliyotolewa kwa kila darasa itosheleze kumaliza ujenzi huo ambapo amewataka Wasimamizi wa miradi hiyo kuhakikisha kuwa kia darasa ndani kunakuwepo na viti na meza kwa ajili ya Wanafunzi.

Akiwa Manipaa ya Mpanda Mkuu wa Mkoa Bi Mwanamvua Mrindoko amekagua Ujenzi wa Vyumba vya madarasa katika Shule za Sekondari Lyamba,Rungwa,Shanwe,pamoja na Mpanda.

Matangazo

  • MWALIKO WA KOTESHENI YA ZABUNI YA KUENDESHA MGAHAWA April 21, 2022
  • ORODHA YA WALICHAGULIWA KUFANYA KAZI YA ANUANI ZA MAKAZI March 28, 2022
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA July 28, 2022
  • FOMU YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA KWA SHULE ZA MANISPAA YA MPANDA December 01, 2021
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • MANISPAA YA MPANDA YAKABIDHI MADARASA 51

    December 28, 2022
  • WASINDIKAJI WAWEZESHWA MIUNDOMBINU NA MASHINE

    November 16, 2022
  • RC KATAVI ARIDHISHWA NA UJENZI WA MADARASA MPANDA

    November 09, 2022
  • SENDIGA AKOSHWA NA HATUA ZA UJENZI WA MADARASA MANISPAA YA MPANDA

    October 25, 2022
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.