Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa ndugu Charles Francis Kabeho mapema leo amezidua zahanati katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kata ya Misunkumilo kijiji cha Milala ikiwa ni juhudi za serikali za kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Ujenzi wa Zahanati ya Milala uliibuliwa na Wananchi kwa lengo la kusogeza huduma kwa Wananchi, kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma ya Mama na Mtoto. Imeelezwa kuwa Zahanati hii inahudumia Wananchi wapatao 7,174 na inalenga kupunguza vifo vya kinamama Wajawazito na Watoto wenye umri chini miaka mitano ambao awali walitembea zaidi ya Km 8 kufuata huduma za Afya katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda.
Aidha Mradi huu mpaka umekamilika umegharimu kiasi cha Tshs. 37,000,000.00 kati ya fedha hizo,Tshs 31,000,000.00 ni fedha toka Serikali kuu kupitia Ruzuku ya Maendeleo (LGDG), Tshs 1,000,000.00 toka Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa na Mchango wa Wananchi ni Tshs. 5,000,000.00.
Katika kutekeleza Mradi huu, kazi zilizofanyika ni kukamilisha ujenzi wa jengo lenye chumba cha Mganga, chumba cha Chanjo, chumba cha kujifungulia, Choo cha kisasa, Stoo ya Dawa, Samani za ndani na Vifaa vya Kitabibu Pamoja na kufunga mfumo wa Umeme wa jua.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.