• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

Viongozi wa Kata, Vijiji, Mitaa wapikwa juu malipo ya ‘TASAF’

Posted on: June 21st, 2018

“Malipo kwa njia ya mtandao, ni rahisi, salama na humfikia mlengwa kwa wakati”. Alisema Lilian Charles Matinga Mkuu wa Wilaya ya Mpanda wakati wa ufunguzi wa wa semina kwa viongozi ngazi ya Kata, Vijiji na Mitaa iliyofanyika jana katika ukumbi wa  Mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.

Aidha amewataka viongozi hao kuwa mabalozi wazuri wa kufikisha ujumbe na elimu kwa jamii wanayoingoza ili kila mlengwa aweze kujiunga na malipo kwa njia ya mtandao.

Akiongea katika mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TASAF makao makuu Bi Anzanuke Mselela ambaye pia ni muwezeshaji wa semina hiyo alianza kwa  kutoa utangulizi na dhana nzima ya TASAF ambapo alisema “Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) ulianzisha mpango wa awamu ya tatu wa kunusuru kaya masikini  kwa kuziwezesha kaya masikini zilizoandikishwa kupata ruzuku ili kumudu mahitaji ya chakula,elimu, afya, lishe bora kwa watoto na kuwekeza katika miradi ya ujasiriamali”

Aidha wakati wa mafunzo bi Anzanuke aliwaeleza wajumbe kuwa TASAF iliteua Halmashauri chache za kufanyia majaribio juu ya malipo kwa njia ya mtandao ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ilichaguliwa kwa ajili ya kuanza kutoa malipo kwa walengwa kwa njia ya mtandao.

Aliendelea kuwaeleza wajumbe kuwa mfumo huo ni rafiki kwa walengwa kwa kuwa wao wenyewe huchagua mtandao au taasisi ya kifedha ambayo ni rahisi kwao kwa ajili ya kupokelea fedha zao. Hadi kufikia mwezi wa tano ni asilimia 37 tu ya walengwa ambao wamejiunga na malipo kwa njia ya mtandao kati ya walengwa 1,501.

Aidha aliwaeleza wajumbe ya semina kuwa malipo kwa njia ya mtandao ni salama kwa kuwa huongeza usalama wa fedha zao kwa  kuwawezesha walengwa kupokea pesa moja kwa moja katika akaunti zao za simu au benki, mahali popote walipo bila kusubiri na kupanga foleni. Pia Yatatoa fursa ya kifikiri na kufanya maamuzi sahihi katika matumizi ya huduma za kifedha ili kuboresha maisha yao. M.f. Kulipia Bima, Kuweka akiba na kulipia huduma mbalimbali. Aidha malipo kwa njia ya mtandao yataondoa athari zinazoweza kutokea wakati wa kusafirisha fedha taslimu kuelekea maeneo ya malipo pamoja na Kupunguza gharama za kusafirisha fedha kwa magari kuelekea maeneo ya malipo.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Kitengo cha Tasaf Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda  yamewajengea uwezo viongozi hao juu ya TASAF, malipo kwa njia ya mtandao na faida zake, aidha wameelezwa majukumu yao kama viongozi juu ya kuihamasisha jamii ili waweze kujiunga na malipo kwa njia ya mtandao.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI MANISPAA YA MPANDA

    February 03, 2025
  • RC RINDOKO ASHIRIKI MAZISHI YA AKOFUDKT. LABAN WA KANISA LA NEW HERVEST CHURCH

    February 09, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAACHA HISTORIA, MTOTO AZALIWA AITWA MWENGE

    August 31, 2023
  • DC MPANDA AKUBALI KASI NA UBORA UKARABATI HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA.

    August 31, 2023
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.