Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Amos G. Makalla amewakabidhi Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Katavi jumla ya pikipiki 58. Makabidhiano hayo yamefanyika mapema leo katika ofisi ya za Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda yakihudhuriwa na maafisa elimu na waratibu elimu kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi amewataka waratibu wote waliopata vitendea kazi hivyo kuvitunza ili viendelee kuwasidia katika kutimiza majukumu yao. Amewataka kutumia pikipiki hizo katika kufuatilia masuala ya elimu kama mahudhurio ya wanafunzi na waalimu mashuleni, ufundishaji wa vipindi madarasani pamoja na majukumu mengine.
Aidha mhe. Makalla amewata waratibu waliopata pikipiki hizo kuzitumia kwa kufuata sheria kanuni za matumizi ya vyombo vya serikali pamoja na kuzingatia sheria za usalama barabarani.
“Mimi ninawaagiza waratibu kuzitumia pikipiki hizi kwa kuzingatia sheria na taratibu za matumizi ya vyombo vya serikali na kwa madhumuni yaliyopangwa na si vinginevyo” Alisema Makalla.
Katika taarifa iliyotolewa na katibu tawala wa mkoa inaonesha kuwa wataribu elimu 17 kati ya 58 hawana leseni zinazo waruhusu kuendesha pikipiki. Hivyo amewataka kufuata taratibu za upatikanaji wa leseni na kukata leseni haraka.
Sambamba na makabidhiano hayo Mhe. Makalla ameishukuru selikali na taasisi ya EQUIP-T kwa kuendelea kuweka kipaumbele katika maswala ya elimu.
Ilembo, Kasimba area
Anuani ya Posta: 216, Mpanda
Simu ya Mezani: +255-2529529
Simu: +255-2529529
Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.