• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mpanda Municipal Council
Mpanda Municipal Council

Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Mpanda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mission and Vission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
        • Tasaf
      • Fedha na Biashara
      • Usafishaji na Mazingira
      • Mipango, Takwimu, Uchumi na Tathmini
      • Land and Town Planning
      • Ufugaji na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
    • Kata
    • Streets
  • Fursa za uwezekezaji
    • Vituo vya Utalii
    • Sekta ya Madini
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Uvuvi
    • Sekta ya Kilimo
    • Sekta ya ufugaji
  • Huduma zetu
    • Elimu
      • Rungwa Sekondari
      • Mpanda Girls Sec School
    • Heath
    • Usafi na Mazingira
    • Maji
    • Ardhi na Maliasili
    • Ujenzi na Miundombinu
    • Woman Empowerment
  • Madiwani
    • List of Counciolors
    • Standing Commitees
    • Time table
      • Vikao vya Madiwani
    • Makablasha/Taarifa za Baraza
  • Miradi
    • Miradi inayo tekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • By laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Strategic Plan
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi
    • Speech
    • Albamu
    • Makala

WAVAMIZI NA WAVUVI HARAMU ZIWA TANGANYIKA WAWEKEWA MTEGO.

Posted on: April 8th, 2023

WAVAMIZI NA WAVUVI HARAMU ZIWA TANGANYIKA WAWEKEWA MTEGO.

Makamanda wa Polisi kutoka mikoa ya kanda ya Magharibi ya Rukwa, Katavi na Kigoma leo Aprili 8, 2023 wamekutana na wadau mbalimbali wa sekta ya uvuvi na Taasisi za sekta ya uvuvi katika kikao kazi cha kutathimini na kupanga mikakati ya kudhibiti vitendo vya uhalifu ziwani na uvuvi haramu katika Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika mjini Mpanda katika ukumbi wa Mpanda Social Hall, mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewataka wadau wa sekta ya uvuvi na wananchi kwa ujumla kuwa na uzalendo kwa kutoa taarifa za viashiria vya uvunjifu wa amani na uvuvi haramu katika maziwa hayo.

Aidha, RC Mrindoko amesema Serikali ya awamu ya Sita inajali na kutambua umuhimu wa sekta ya uvuvi na ndiyo maana inaendelea kufanya uwekezaji kwa kujenga mialo hivyo ameliagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi maeneo yote ya Ziwa Rukwa na Ziwa Tanganyika ili kukomesha uhalifu na uvuvi haramu.

Vilevile, ametoa wito kwa wavuvi katika mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma hususani wananchi wa mkoa wa Katavi kuitumia Bandari ya Karema Wilayani Tanganyika kusafirisha mazao yatokanayo na ziwa hilo kwani tayari Bandari imeanza kufanya kazi.

Awali akiwasilisha taarifa kwa mgeni rasmi, CP Awadhi Juma Haji, Kamishna wa oparesheni na mafunzo ya Jeshi la Polisi Tanzania amesema kwa kiasi kikubwa vikao hivyo vinavyofanyika kila baada ya miezi sita vimesaidia kupunguza uvuvi haramu katika maziwa hayo na maziwa mengine Nchini.

Amesema moja ya changamoto walizobaini ni pamoja na baadhi ya wavuvi kuzungukana wao kwa wao kwa kuibiana nyavu kutokana na tamaa za kupata mali haraka, baadhi ya maafisa kupokea rushwa kwa wahalifu na kuvujisha siri za mikakati inayopangwa na Jeshi, kutoshughulikiwa ipasavyo kesi zinazotokana na uvuvi haramu.

Hata hivyo, ametoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na matukio ya kiuhalifu ya kupora nyavu, mitumbwi ikiwemo uvuvi haramu kuacha mara moja kwani Jeshi la Polisi Nchini liko imara na litaendelea kufanya oparesheni ili kuwakamata wote wanaojihusisha na matukio ya uhalifu.

Matangazo

  • THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN MPANDA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 06, 2025
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA December 27, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2024
  • KUITWA KAZINI January 06, 2024
  • Tazama zote..

Habari za Hivi Punde

  • SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

    June 19, 2025
  • SERIKALI YALETA BILIONI 29 MANISPAA YA MPANDA NDANI YA MIAKA 5

    June 19, 2025
  • MADIWANI WAAGA RASMI

    June 19, 2025
  • MADIWANI WAAGA RASMI

    June 19, 2025
  • Tazama zote..

Video

Uzinduzi wa Tovuti mpya kitaifa
Video zaidi.

Kurasa za Haraka

  • Revenue Collection Dashboard for Katavi Region

Tovuti Zinazohusiana

  • TAMISEMI
  • Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

professional Writing Service

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ilembo, Kasimba area

    Anuani ya Posta: 216, Mpanda

    Simu ya Mezani: +255-2529529

    Simu: +255-2529529

    Barua Pepe: md@mpandamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa Mpanda. Haki Zote Zimehifadhiwa.